Mwenyekiti wa mtaa wa Tanesco wilayani mbulu mkoani manyara Joseph Paul ametoa wito kwa wakazi wote wa mtaa huo kulinda mazingira yao.
Akizungumza na kituo hiki,Bw Paul ni vyema wananchi wakatunza mazingira yao hasa vyanzo vya maji ilikujikinga na milipuko ya magonjwa inayoweza kujitokeza.
Mwenyekiti ametoa rai hiyo baada ya mtu mmoja asiye julikana kujisaidia haja kubwa katika kisima cha maji wanachotumia wananchi kwa matumizi ya familia.
Bw Joseph amewaomba wakazi wote wa mtaa huo kuyalinda na kuyatunza mazingira yanayo wazunguka.
Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa mtaa huo wamelaani kitendo hicho na kuiomba serikali kuwashughulikia watu wote wenye tabia kama hizo katika jamii.
Wakazi hao wamewataka watu wote wenye tabia kama hizo kuachana nazo mara moja kwa ustawi wa mazingira yao.