Misaada mbalimbali ya kibinadamu imeanza kuwafikia watu wanaokabiliwa na mahitaji mbalimbali, baada ya nchi ya PERU kukumbwa na mafuriko mabaya zaidi kuliko yote kuwahi kutokea nchini humo miongo miwili iliyopita.

Baadhi ya watu waliolazimika kuyahama makazi yao na kwenda kujihifadhi katika maeneo salama, sasa wameanza kupokea misaada ya maji ya kunywa, huku wakiendelea kusubiri misaada mingine ya kibinadamu ikiwemo ya vyakula.

Zaidi ya watu SABINI NA WATATU wamekufa kutokana na mafuriko hayo yaliyoambatana na maporomoko ya udongo na kulikumba eneo kubwa la nchi ya PERU.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *